Saa chache baada ya Posti ya msanii AliKiba kutweet tweet ambayo inatajwa inamuhusu hasimu wake Diamond Platnumz, ndipo upande wa pili ukajibu mashambulizi kwa kuachia audio yenye Verse 1 kwa kupitia beat ya wimbo ule ule wa Fresh, ambapo ndani yake kamhusisha Kiba na Ommy Dimpoz.
OMMY DIMPOZ AMJIB DIAMOND
Dimpoz baada ya kuusikia wimbo huo, akaamua kuliamsha dude, ambalo ndiyo linazizima mpaka sasa, huku mashabiki wakiwa na shauku ya kutaka kujua upande wa pili utafanya nini.
Katika mahojiano na kituo kimoja cha luninga hapa nchini msanii Shetta amefunguka kuhusu beef za wasanii zinazoendelea na kushauri ni vyema zikawa ni beef za kibiashara na siyo kuwekeana uhasama kwenye maisha ya kawaida.
Post a Comment