banner

Tuesday, November 7, 2023

SIMBA YAVUNJA MKATABA NA KOCHA WAKE

SIMBA YAVUNJA MKATABA NA KOCHA WAKE

 Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya pande zote mbili ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza Roberto Oliveira Goncalves Do Carmo (Robetinho).



Taarifa iliyotolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Iman Kajula imesema Klabu hiyo imefikia pia makubaliano ya kusitisha mkataba wa kocha wa viungo Corneille Hategekimana.


“Uongozi wa Klabu ya Simba unawashukuru Makocha hawa kwa mchango wa ndani ya klabu yetu na inawatakia kila la heri katika majukumu yao mapya, katika kipindi cha mpito kikosi chetu kitakuwa chini ya Kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Seleman Matola na tayari mchakato wa kutafuta Makocha wapya umeanza na unatarajiwa kukamilika hivi punde”


Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search