MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, amesema yupo katika mipango ya kuhakikisha Wafanyabiashara wote waliopo Machinjioni wanaingia katika Databases ( kumbukumbu za utambuzi).
DC Mjema ameyasema hayo leo kwenye ziara yake Mara alipotembelea Machinjio hayo ili kuona kero zinazowakabili.
Aidha, DC Mjema, amesema anataka kuona Wafanyabiashara hao hawapati shida na kunyanyaswa kwa kuwa Serikali ya awamu ya tano ipo kwa ajili yao.
"Nataka mtembee kifua mbele na kuacha dhana ya kudharauliwa kwani mnategemewa katika Serikali ya Wanyonge" Amesema DC Mjema.
Amesema wakati wanakwenda kuingia kwenye Machinjio ya kisasa lazima wajue wanakwenda kufanya kazi wapi na vipaumbele vitolewe kwa Wafanyabiashara husika.
Amesema Wafanyabiashara wa Machinjio wanakila sababu ya kuhalalishwa kwakuwa wanachangia pato kubwa katika Manispaa ya Ilala.
Katika hatua nyingine, amesema eneo litakalo jengwa Machinjio ya kisasa litakuwa na eneo la Mita za mraba Elfu Ishirini ambapo Mita 10 za mraba waangalie kutenga eneo la Wafanyabiashara wa nje wanafuata Nyama.
Akijibu tuhuma za Wakina mama kukaa nje na kulala wakizuiwa kuingia ndani, amesema kuwa kwa sasa ruksa kuingia lakini wafuate kile walichokifuata.
Akizungumzia kuhusu kuporomoka kwa bei ya ngozi ,amemtaka Kiongozi anayeshikilia idara hiyo ahakikishe mpaka kufikia tarehe 26 mwezi 10 wakae ili kuandaa mpango wa wa semina ya ngozi kwa Wafanyabiashara ili kuona Serikali itaingiza kiasi gani na wao ili kulinda maslahi katika Biashara zao.
Kero ya Maji, amesema kesho DAWASA wataenda kuangalia jinsi ya kuwasaidia lakini amewatahadharisha kuhusu uzwaji wa Maji hayo na watakao bainika watachukuliwa hatua.
Total Pageviews
Popular Posts
-
Miongoni mwa Picha maarufu mitandaoni ni hii ya Mfalme wa Pop marehemu #MichaelJackson na Hayati Ali Hassan Mwinyi ambaye hapo alikuwa Rais ...
-
Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ametoa ahadi ya kuwataja wote walioko nyuma ya ufisadi wa Kampuni ya ufuaji umeme ya Independe...
-
Katika kuelekea mchezo wa Ndondi kati ya Mtanzania na Mtumishi wa JWTZ Sajinitati Selemani Kidunda (JINI MAKATA) na Bondia Kutoka nchini Afr...
-
"Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa. Mheshimiwa Lowassa ameitu...
Post a Comment