WAFANYA Biashara ya Mifugo katika Machinjio ya Vingunguti wamelalamikia Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh: Sophia Mjema, kutoshirikishwa katika maamuzi juu ya utendaji unaofanyika katika Machinjio hayo.
Wakizungumza na waandishi wa Habari kwa nyakati tofauti tofauti leo kwenye ziara ya Mkuu wa Wilaya ikiwa ni kutatua kero za Wananchi (Majina yao yamehifadhiwa) , wamesema kuna mambo ya hovyo yanayofanywa na Watendaji wao hawaridhishiwi nayo kutokana na kutoshirikishwa katika shughuli zinazofanyika katika Machinjio hayo.
Naye , Kaimu Afisa Mfawidhi Machinjio ya Vingunguti, Mgeni Abdallah, amesema Chinjio hilo linachangamoto sana hivyo wamemuomba Mkuu wa Wilaya ya Ilala kuwasaidia kutatua kero zao.
Aidha katika kutoa taarifa fupi ya Machinjio, Mfawidhi Mgeni, amesema Machinjio hayo yalianziashwa 1959 wakiwa na wastani kuchinja Ng'ombe 25-30, na mbuzi.
Pia amesema kwa sasa wanachinja Ngo'mbe 500 hadi 600 na Kondoo 400 hadi 450 kwa siku ambapo ni tofauti na awali.
" Tunashukuru sana ,Dc Mjema, kwa kuja hapa kutusikiliza sisi bado tupo katika hali mbaya hivyo Machinjo ya kisasa tunaimani mambo yatakuwa mazuri "Amesema Mgeni.
Aidha katika hotuba yao, wamesema katika mwaka wa bajeti ya mwaka 2015/2016 walikusanya milioni 634, mwaka 2016/2017 milioni 771 na mwaka 2017 hadi kufikia mwezi Juni 2018 milioni 920.
Katika kuelezea changamoto, amesema idadi kubwa ya watu na baadhi yao wakiwa hawana shughuli maalumu ina punguza malengo waliojiwekea.
Pia uwepo wa miundombinu mibovu unachangia kutokuwepo kwa huduma rafiki kwa wateja.
Aidha amezitaja shughuli mbali mbali wanazozifanya ikiwamo shughuli za ukaguzi wa awali wa Nyama, pamoja na ukusanyaji wa ushuru wa Machinjio.
Total Pageviews
Popular Posts
-
Msanii wa hiphop, Rosary Robert ‘Rosa Ree’ ameamua kuachana na ulevi wa pombe baada ya kugundua haina faida katika maisha yake. Msanii hu...
-
Msanii wa muziki, Mrisho Mpoto ambaye pia ni Balozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro baada ya wiki hii kuachia wimbo wake mpya ‘Kitenda...
-
Uamuzi wa kupokea au kutopokea kielelezo cha ushahidi cha msokoto mmoja wa bangi na vipisi viwili vya bangi katika kesi inayomkabili mlimbw...
-
Miongoni mwa magonjwa ambayo husumbua watu wengi kwa kiwango kikubwa ni moyo, hivyo ili kuweza kulinda afya ya moyo wako ili usipate mago...
-
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, Ulrich Matei amesema wana washikilia watu wanne kwa tuhuma za kukutwa na bastola moja yenye risas...
Post a Comment