MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, amesema Mgambo hawana mamlaka ya kukagua vyoo na kuingia ndani kwa mtu kwani wenye jukumu hilo ni Bwana Afya na Bibi Afya nasivinginevyo.
Amesema kuwa zipo taarifa nyingi za malalamiko kuhusiana na mgambo kwamba wanawanyanyasa kuwapiga na kuwatoza faini sasa hizo kero hataki kuzisikia.
"Ndugu zangu kazi ya mgambo ni kuwaelekeza Wananchi jinsi ya kufanya usafi na baada ya hapo watakao kaidi walipishwe faini ila sio wanafika tu wanatoza faini bila kuwapa Elimu ya usafi"amesema DC Mjema.
Amesema suala la taka taka ni changamoto kwa kuwa wamebakia na magari machache ambapo mengine ni tenda kwa walioomba kufanya usafi hivyo katika kuona suala hilo linafanyiwa kazi wamejipanga kuleta magari 5 yatakayo hudumia Kata ya Gongolamboto, Minazi mirefu, Kiwalani pamoja na kipawa ili kupunguza asilimia 55% ya taka inayobakia mitaani.
Amesema Serikali inampango wa kuhakikisha taka taka zote zinageuka dili kwa kuja na mfumo wa kugeuza taka taka ngumu kufanyiwa cycling na zile nyingine kuchomwa ili. Kupata gesi mbadala.
Mbali na kero za usafi, amezungumzia suala la ulinzi Shirikishi huku akisema kuwa lazima wananchi watambue umuhimu wa ulinzi shirikishi na kulipa Pesa walizokuliana ili kuwasaidia wale waliojitolea kuwalinda.
Pia katika hatua nyingine amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa kumtafuta mkandarasi aliyejenga Mradi wa Maji uliopo Kata ya Minazi mirefu ili alipie gharama hizo za ujenzi upyaa maana mradi haujakizi vigezo na wale wote waliohusika na kukwamisha huo mradi wachukuliwe hatua.
"Mradi huu ni wa muda mrefu sana japo hizo kero za kukosekana kwa mfumo wa miundombinu lakini bado Nina mashaka na waliohusika sasa Mkurugenzi hakikisha watu Hawa wanapatikana na kutujibu "amesema DC Mjema.
Katika hatua nyingine , Dc Mjema , amemuagiza RPC , kuwakamata wale walio na makanisa ambayo hawana kibali yafungwe.
Amesema yapo makanisa yanayopiga mziki masaa 24 hivyo yaache haraka sana tabia hiyo.
" Rpc nakuagiza kamata wale wote wanaoanzisha makanisa na kufanya ibada SIKU zote za kazi kwa kutumia mziki, huu sio utaratibu Bali tunawatesa wenzetu kuna watu wanahitaji kupumzika watoto wanahitaji kisoma, he watasoma muda gani? Sasa kuanzia Leo tunaanza operesheni ya ukaguzi huo Mara moja ili kuwabaini watu hao" amesema Dc Mjema.
Bar zinazopiga mziki masaa 24 ambazo hazina leseni ziache Mara moja hatua Kali za kisheria zitachukuliwa zidi yao.
Total Pageviews
Popular Posts
-
Msanii wa hiphop, Rosary Robert ‘Rosa Ree’ ameamua kuachana na ulevi wa pombe baada ya kugundua haina faida katika maisha yake. Msanii hu...
-
Msanii wa muziki, Mrisho Mpoto ambaye pia ni Balozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro baada ya wiki hii kuachia wimbo wake mpya ‘Kitenda...
-
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemtaka Msanii Whozu @whozu_ kushusha mara moja video ya wimbo wake wa ‘Ameyatimba’ kwenye digital plat...
-
Uamuzi wa kupokea au kutopokea kielelezo cha ushahidi cha msokoto mmoja wa bangi na vipisi viwili vya bangi katika kesi inayomkabili mlimbw...
-
Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya pande zote mbili ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza Roberto Oliveira Goncalves Do...
Post a Comment